Tuesday 25 October 2016

Abiria kituo cha Tegeta nyuki walia na Halmashauri.

Na Peter Mhina.

    Abiria  katika kituo cha dala dala  cha tegeta nyuki wameilalamikia  halimashauri ya  wilaya ya kinondoni ,kwa kushindwa kukarabati kituo hicho ikiwa ni pamoja na  ukosefu wa sehemu za kusubiria usafiri ,jambo ambalo limekuwa kero  hasa pale mvua inapo nyesha na wakati wa kiangazi  







  Akizungumza kwa nyakati tofauti hapo jana kituoni hapo abiria huyo aliyaelekeza  makucha yao kwa viongozi wa halimashauri  huku baadhi yao wakiutupia mpira uongiozi wa kituo hicho kutokana kwa kushindwa kuweka mikakati inayoeleweka kituoni hapo


‘’Nitatizo kubwa kwasababu ukija kuangalia hakuna sehemu ya kukaa ambayo unaweza kujikinga na jua ama mvua endepoitakapo kuja kunyesha na muda mwingine  unaweza ukaja kuomba wenye vibanda pembembeni  wanaofanya biashara kujiegama   ukawa unawakera vile vile,’’  Alisema mmoja wa abiria hao ,



  Pia kwa upande wa madereva  katika kituo hicho  wametaka halimashauri kukifanyia malekebisho upya kituo hicho ikiwa ni pamoja na ubovu wasehemu wanapo paki daladala kutokana na kuwepo kwa mashimo jambo linalowapa shida wakati wa masika  na hivyo kupelekea magari yao kuharibika  kila wakati .


‘’Tunaumia sana kutokana na  tunachangishwa ela kila siku lakini mabadiliko  hakuna, huwa kuna bomba likipasuka maji yanajaa  na kusababisha mashimo  na magari yetu yanazidi kuumia  alafu pesa nyingi tunatoa  hamna mabadiliko yoyote katika kituo hiki,’’ Alisema mmoja wa madereva hao.

 Wakati huo mwandishi wetu  ilijaribu kwa hali na mali  kuwatafuta wa husika na ilipofika ofisi za kituo hicho  wahusika hawakuonesha ushilikiano huku ofisi hizo zikionekana kufugwa licha ya wahusika kuwepo mahali hapo .

 Kituo cha daladala cha tegeta nyuki  kilianzishwa lasimi mwaka 2013.,Licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa zinazokabiri kituo hicho   bado kimendelea  kuwa kitovu cha usafiri kwa wakazi wa tegeta na maeneo ya kando kando kutokana na kupatikana kiurahisi usafiri wa kuwapeleka sehemu tofauti tofauti za katikati ya mji na maeneo mengine ya jiji la Dar es salaam.


  

No comments:

Post a Comment