Thursday 27 October 2016

MDEE AWATIA MOYO WAKAZI WA TEGETA MASHIMO YA MAWE



Na Christian John
Baada ya mgogoro wa muda mrefu bain ya serikali na wakazi wa Tegeta machimbo ya mawe sakata hilo limehamia kwa Mbunge wa Jimbo hilo la Kawe Mh.Halima Mdee na kuzungumza na wananchi wa maeneo  hayo.
Akizungumza hayo katika ziara aliyoifanya eneo hilokwa lengo la kujua matatizo yanayowakabili wananchi wake Mdee amewatia moyo kwa kuwaambia atapigana kwa kadiri anavyoweza kuhakikisha wanapata haki yao.
"Wanasema nyie ni wavamizi lakini hakuna mvamizi kwenye nchi yake nyie mna haki ya kuwa hapa kuna watu wana miaka zaidi ya ishirini maeneo haya wameoa na wana wajukuu  nyie niwamiliki halali kabisa"
Baada ya kuulizwa kuhusu kauli hiyo na huenda ikamletea matatizo kwa kuikashifu serikali alisema
"Hakuna wa kuikashifu serikali wala kuidharau ila tunaongea ukweli ambao upo wazi kabisa ili mradi hatujatukana basi tujue wazi tuna haki"
Kwa muda mrefu sasa serikali imekuwa katika mgogoro na wakazi wa eneo hilo kwa kile kinachodaiwa wakazi hao kuvamia eneo hilo ambalo halijapimwa na manispaa.



No comments:

Post a Comment