Thursday 27 October 2016

Wazawa wagoma kutalii

Na Mari Kilua

Swala la wazawa kutembelea vivutio bado imekuwa changamoto ndani ya hifadhi nyingi nchini Tanzania pamoja na kwamba Tanzania ni moja ya nchi zinazoongoza kwa vivutio vingi vya utalii



Akizungumza na waandishi wa habari kutoka Tsj mmoja kati ya waongoza wageni ndani ya hifadhi ya Ngorongoro George Okol amesema "tumekuwa tukipokea watalii wa kigeni zaidi kuliko wazawa na hii inaonesha ni jinsi gani watanzania tunashindwa kijani kujari cha kwetu".

Pia mmoja wa watalii wa ndani ambaye alikuwa ndani ya hifadhi hiyo amesema "kiukweli inatia aibu sana kwa swala la wageni kuwa wengi kuliko wazawa, cha msingi serikali pamoja na waandishi mnatakiwa kufikisha elimu ya kutosha kwa watanzania ilikuweza kutoka kwenye janga hili", amesema mmoja ya watalii ambaye hakutaka kutaja jina lake.


Baadhi ya wazawa wameileza jsj kuwa sababu inayowafanya washindwe kutembelea hifadhi zao ni kutokana na bei kubwa ya kiingilio ikijumulishwa na pesa ya kulipia kula kitu ndani ya vivutio hivyo


Nayo mamlaka ya hifadhi ya taifa ya utalii imeeleza kuwa watajiatahidi kupunguza kiingilio kwa watalii wa ndani ili kuweza kuwatia moyo zaidi watalii hao.

No comments:

Post a Comment