Wananchi wa mtaa wa Sharifushamba wamelalamikia uwepo wa malori na mabasi yanayoizidi uwezo barabara iliyopo mtaani hapo.Wakizungumza na chombo hichi wengi wameonekana kuchukizwa na uwepo wa malori na kusababisha msongamano usio na maana katika barabara hiyo.
BASI LINALOMILIKIWA NA KAMPUNI YA SARATOGA LIKIWA LIMEEGESHWA NJIANI |
Mtaa wa sharifushamba ni moja kati ya mitaa yenye bahati kujengewa barabara zenye kiwango cha lami.Kutokana na uwepo wa malori na mabasi makubwa na kukosekana kwa maegesho ya magari kupita katika barabara hiyo,hivyo imekuwa kero kwa baadhi ya watumiaji wa barabara hiyo hasusani wakazi wa maeneo hayo.
Baadhi ya wananchi wanaokaa katika mtaa huo wameeleza kero yao kubwa huku mmoja kati yao ambaye anafahamika kwa jina la Munga jina kamili Said Munga alisema kuwa kero yake kubwa ni uwepo wa malori yaliyozidi uwezo wa barabara hiyo kwani barabara hiyo imejengwa maalumu kwa magari yenye tani 10 mpaka 15 lakini cha kushangaza mpka mabasi makubwa yanapaki na kupakia mizigo eneo hilo.
LORI LINALOMILIKIWA NA KAMPUNI YA BACK TOWN LIKIJARIBU KUPITA KATIKA BARABARA HIYO AMBAYO IKO MTAANI AMANA SHARIFUSHAMBA PEMBEZONI KUNA MAKAZI YA WATU |
BAADHI YA MAGARI YAKIWA YAMEEGESHWA PEMEBEZONI MWA BARABARA INAYOPITA MTAA WA AMANA SHARIFUSHAMBA |
Hata hivyo kutokana na uwepo wa nyumba ya kulala wageni jirani na eneo hilo na ukizingatia nyumba hiyo haina sehemu ya kuegeshea magari na hivyo kupelekea msongamano ambao mara nyingi huwa nio kero kwa watumiaji wa barabara hiyo kwani barabara hiyo ni nyembamba sana.Hivyo ilinibidi kuzungumza na mmiliki wa nyumba hiyo lakini juhudi za kumpata ziligonga mwamba.
No comments:
Post a Comment