Friday 28 October 2016

WANANCHI WA JIJI LA DAR ES SALAAM WAIPONGEZA SERIKALI


NA ANNA J. MUNISI
Wananchi na wakazi wa jiji la Dar es salaam  hasa wale wanaotumia barabara ya TAZARA wamefurahishwa  na kitendo cha serikali kutekeleza ujenzi wa barabara hiyo  ambayo ilikuwa ikilalamikiwa kuwa na adha kubwa ya foleni.
Awali wananchi na madereva wanao tumia barabara hiyo walikuwa wakipata shida sana kupita katika barabara hiyo kutokana na msongamano mkubwa wa magari na hivyo kuchelewa mahali wanapokwenda.

Akizungumza na mwandishi wetu mmoja waabiria  alisema “ unajua sasahivi wanatupa moyo kidogo kwa kuuona ujenzi wa barabara mpya nadhani itatusaidia sana siku za mbeleni kwani tumekuwa tukifika majumbani usiku sana kutokana na eneo hili kuwa na foleni kubwa” alisema  mmoja wa abiria ambaye hakutaka jina lake lifahamike.
Naye Bw. Hashim Kareem alisema “tunatamani sana ujenzi huu ukamilike ili foleni zipungue, watu wanachelew kazini na wengine wanafika nyakati za usiku sana majumbani hii si nzurio kwani tunahatarisha maisha yetu kutokana na vibaka ambao wanazurura usiku”.

Aidha mmoja ya wakandarasi wa eneo hilo Christian Joseph amabae anashughulika na ujenzi  huo wa barabara alitoa ufafanuzi kuhusiana na barabara hiyo ya TAZARA  kuwa ujenzi utakamilika ifikapo mwaka 2018 na barabara hizo zitakuwa ni za juu na chini ili kupunguza foleni ya magari, kutakuwa na barabara maalumu kwaajili ya magari makubwa na nyinginekwaajili ya magari ya kawaida.




No comments:

Post a Comment