Thursday 27 October 2016

MAJI TAKA KERO KUBWA KWA WANANCHI WA SPENKO


NA NAJAT  ATHUMANI.
  WAKAZI wa eneo la Spenko Vingunguti wamelalamikia uongozi wa eneo hilo kwa kuto kupuliziwa dawa  kwenye mabwawa ya maji taka jambo linalopelekea kugeuka mazalia ya mbu pamoja nakutoa harufu kali wamesema hayo walipo tembelewa na mwandishi wetu jana.
Wamesema kumekuwa na kawaida ya baadhi ya viongozi wanao husika kulipuuzia swala hilo kwa kutokufuata utaratibu ulio wekwa na serikari wa kuhakikisha mabwawa  yanapuliziwa dawa kila baada ya muda mfupi swala linalopelekea kero kubwa kwa wakazi hao.

"Mwanzoni walikua na utaratibu mzuri  walikua wanapulizia dawa kila baada ya muda mfupi lakini sasa wamekuwa wanafanya wanapojisikia swala linalokua kero kwetu hasa nyakazi za mchana jua linapo waka hua kunakuwa na harufu kalii na nyakati za usiku mbu wanakuwa wengi mno”  alsema  mmoja wa wakazi wa eneo hilo anayejulikana kwa jina la Elizabeth Mlawa.

Naye  mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo Bw Omary said Omary naye alikua na haya yakusema "mimi napokea malalamiko mengi mpaka nakosa raha nikweli kunatatizo hilo namimi najitahidi kadri ya niwezavyo kulishugulikia napia kumekua na mzunguko mkubwa wa kupatatikana kwa dawa hizo mwanzo kulikuwepo shiriika kutoka marekani lililo kuwa na kampeni ya kuzui Malaria ambalo ndio lililokua linapulizia dawa hivyo baada yakuondoka kumekua nashida kwakweli". alisema
Juhudi  bado zinaendelea  za kumtafuta meya wa jiji kutolea ufafanuzi wa kina juu ya suala hili linalowakerehesha wakazi wa spenko kwani mbu wanaozalishwa na bwawa hilo wanachangia kwa kiasi kikubwa kusabisha kuongezeka kwa idadi ya maambukizi ya ugonjwa wa malaria hasa kwa  watoto chini ya miaka mitano na wamama wajawazito.

Pichani  ni makazi ya watu yalio karibu na bwawa la maji taka spenko

Baadhi ya wakazi wa spenko wakiendendea na shughuli zao za kila siku pembezoni mwa mabwawa ya maji taka

Picha ikionesha muonekana halisi wa mabwawa ya maji taka yaliyopo vingunguti mtaa wa spenko.
PICHA NA NAJAT ATHUMANI.



No comments:

Post a Comment