Thursday 27 October 2016

HEKA HEKA KWA MACHINGA



Na ANITHA JAIL

Wafanyabiashara ndogo ndogo(machinga)wamepatwa na sintofahamu baada ya wagambo wakishirikiana na polisi kuwafukuza katika maeneo ambayo sio sahihi kufanyia biashara

Machinga washatangaziwa kuacha kufanya shughuli zao kwa kupanga barabarani hususani barabara ya mabasi yaendayo haraka katika mitaa ya Kariakoo na Mnazi mmoja ili kupunguza msongamano wa watu mjini

Wafanyabiashara wamepata hasara ya vitu vyao kwani Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi ili kuwaondoa katika eneo hilo

Wagambo wa jiji wakishirikiana na mapolisi wametanda kila kona ya mitaa ya Kariakoo kupambana na machinga ambao wameambiwa wahame maeneo hayo
 
Baada ya tamko hilo wamachinga wamekataa wamedai haiwezekani tutapambana nao kwani hawana maeneo ya kufanyia bishara zao
Licha ya vitu vyao kuharibiwa baadhi ya machinga walipata majeraha katika harakati za kuokoa mali zao

‘Nategemea  na napoteza muda mwingi kufanya biashara hii kukidhi mahitaji ya kifamilia na kusomesha watoto wanavyotufukuza hatuna sehemu nyingine ya kufanyia biashara’Alisema mmoja wa wafanyabiashara hao

No comments:

Post a Comment