Wednesday 26 October 2016

TSJ YATOA MSAADA SHULE YA MSINGI LAIBONI.

Na  Sabore Laizer

Chuo cha Uandishi wa habari Time school of journalism kilichopo jijini Dar es salaam kilitembelea shule ya msingi LAIBONI iliyopo kata ya makuyuni wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha na kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa mwanafunzi .



Mratibu wa masomo katika chuo cha Tsj Bi Blandina Semaganga alisema serikali ya mwanafunzi ikishirikiana na uongozi wa Chuo iliandaa zawadi kidogo kwa ajili ya mwanafunzi ikiwemo madafutari kalamu box sita, katoni nne, sabuni katoni tano, na sabuni ya unga box moja lenye zaidi ya vipande miamoja .


Mkuu wa shule hiyo Bi Rogath mbuya alishukuru uongozi wa chuo cha Tsj kwa msaada hiyo,vilevile alibanisha changamoto mbalimbali katika shule ya ke kuwa wanatatizo la maji has a kipindi hiki cha kiangazi wanalazimika kununua maji kwa ajili ya matumizi ya shule.

                               
Bi mbuya aliongeza kuwa boza ya Lita mia tatu inagharimu shilingi laki mbili kutoka Mto wa mbu ambapo maji hayo yanatumika katika shughuli mbalimbali shuleni hapo ikiwemo kupikia ,kudeki madarasa na usafi vyooni.


Pia Bi mbuya alisema kuwa wanapata pesa ya kununua maji kupitia michango kwa wazazi na wafadhili kutoka sehemu mbalimbali na vile vile pindi maji yanapokosekana shuleni mwanafunzi hushinda njaa kuanzia saa moja asubuhi hadi saa kumi jioni watakaporudi nyumbani.



Licha ya kukumbana na changamoto mbalimbali shule ya LAIBONI ni ya kipekee ambapo ilianzishwa 1997 na Mganga wa jadi Mzee Meshuko Mapi kwa ajili ya familia take na watoto wa jirani.

No comments:

Post a Comment