Thursday 27 October 2016

WAKAZI WA BUGURUNI WAIPONGEZA SERIKALI KWA UTEKELEZAJI WA AHADI




NA NAJAT ATHUMANI.
Wafanya biashara wa eneo la buguruni wameishukuru serikali kwa kufanikisha ujenzi wa kivuko cha juu kilichomalizika mwishoni mwa wiki jana jambo linalowasaidia wakazi hao kuvuka kwa urahisi kutoka upandemmoja kuelekea mwingine bila bugudha yoyote.
Mwandishi wetu alishuhudia hayo alipotinga  eneo ambalo lipo daraja hilo  ili kushuhudia na kupata maoni ya wananchi kuhusu kivuko hicho huku wengi wakionesha furaha yao kwa utekelezaji wa jambo hilo.
 ‘‘ Kivuko hiki kimetusaidia sana kwasababu tulikuwa tunapata shida kuvuka barabara kutokana na kasi ya madereva wa vyombo vya moto mara nyingi wanapita kwa kasi sana kwakweli serikali imetuona’’alisema mmoja wa wafanyabiashara waeneo hilo anayejulikana kwa jina la Sayde Othuman.
‘‘ hiki kivuko ni chetu tumejenga kwa kwa kodi zetu lakini cha kushangaza wachache watakitumia vibaya  ndani ya mwezi tu wataanza kung’oa vyuma  serikali iangalie hilo sio kwasababu wamemaliza basi wakiiche tu watu tunatofautiana uelewa’’ alisema Michael  Kasoni mkazi wa buguruni.
Pia tuliongea na askari wa barabarani aliyekuwa zamu  kuongoza magari eneo hilo alisema eneo hilo huwa linakluwa na foleni kubwa jambo linalowafanya wavukaji kuvuka pindi magari yanapokuwa kwenye foleni huku waendesha pikipiki wakipita kwa kasi pembezoni mwamagari hivyo kuhatarisha maisha ya wananchi wanaovuka katika hiyo barabara.
‘‘boda doda wanakatisha kwa kasi pembezoni mwa magari yakiwa yamesimama kusubiri ruhusa mtu akikatisha vibaya lazima apitiwe na pikipiki,kwasasa  kuna nafuu maana wanafunzi ndio walikuwa wanapata shida kuvuka sasa wanapanda tu kivuko wanavuka kirahisi wahusika wamejitahidi na mimi wito wangu ni kwa wananchi kukitunza kivuko hicho na siyo hicho tu bali na miundombinu yote inayotusaidia hasa ya barabarani ili iweze kutusaidia’’ alisema askari huyo.
Ni siku chache zimepita tangu kutokea ajali iliyosababishwa na dereva wa pikipiki  kugongana na gari kubwa aina ya fuso tukio lililopelekea bibi aliyekuwa akivuka katika barabara hiyo kugongwa na kupeteza maisha.hivyo kuwepo kwa ujenzi wa kivuko cha daraja hilo kutasababisha kupungua kwa ajali.
Hili ni daraja ambalo linatumika kama kivuko salama kwa wakazi wa buguruni jijini dare s salaam

No comments:

Post a Comment