Thursday 27 October 2016

TSJ YAPATA FURSA SUNRISE RADIO



Na Fatuma Sultani

Chuo cha uandishi wa habari TIME SCHOOL OF JOURNALISM kilichopo jijini dare s salaam kimepata fursa ya kuajiriwa sunrise redio pindi wakimaliza masomo yao na pia baadhi ya wanafunzi wamepewa nafasi ya kuweza kufanya uwandani ndani ya radio hiyo.

Tukio hilo lilijiri hivi karibuni wakati wanafunzi wa chuo hicho walipokuwa kwenye ziara yao ya kimasomo mkoani ARUSHA, na kuamua kutembelea kituo hicho cha habari kwa lengo la kujifunza kwa vitendo zaidi na kuona nini ambacho wenzao huwa wanafanya pindi wawapo makazini.


Baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho walifurahi sana kuwepo kwenye radio hiyo kwani wameweza kujifunza mambo mbalimbali redio hapo,na pia walipata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali kuhusu fani yao na walibahatika kuona vitu kwa vitendo.
  

Mkurugenzi wa radio hiyo alisema kuwa anashukuru uongozi wa chuo cha TSJ  kwa kuchagua redio yao kwani wamefarijika sana na kuona kuwa kazi wanayoifanya ni kubwa na jamii huwa wanaikubali na wanaelimika juu ya mambo wanayoyafanya.
   


Mkuu wa chuo hicho Bi SUZAN LUKA alituma salamu za kuwashukuru uongozi wa sunrise redio kwa kukubali ombi lao la kutembelea kituo hicho na pia kuwashukuru kwa kuonesha ushirikiano wa hali ya juu ya kuwakubalia wanafunzi kwenda kufanya uwandani redioni hapo kuwaahidi kupata nafasi pindi wamalizapo elimu ya diploma chuoni hapo.

No comments:

Post a Comment