Friday 28 October 2016

WAKAZI WA VINGUNGUTI WALALAMIKIA UKOSEFU WA KITUO CHA DALADALA



Wakazi wa vingunguti  jijini  Dar es salaam  wamelalamika kwa kukosa kituo cha daladala kwa muda mrefu  sasa hali inayopelekea kuwa na wakati mgumu kipindi wanapokua wanafuata huduma za usafili hususani kipindi cha masika kwa sababu hulazimika kulowana na mvua kwa kukosa sehemu za kujistili ili wasiweze kuloweshwa na mvua vilevile majira ya kiangazi hususani mida ya mchana kwa kuchomwa na jua kali.


Licha ya kupeleka malalamiko hayo katika sehemu husika na kufanya jitihada kadha wa kadha ikiwemo kumtumia  ujumbe diwani wa kata hiyo na viongozi wengine lakini jitihada hizo azikuzaa matunda.

Isihaka Issa mkazi wa vingunguti alikuwa na haya ya  kuelezea dhidi  ya kero hiyo wanayoikumbana nayo ‘’  muda mrefu sasa tangu sisi wakazi wa huku vingunguti  tuanze kuitumia  barabara hii ambayo ilijengwa bila kuwepo na vituo vya kupumzikia abiria,


Vile vile Bw. Isihaka Issa aliongeza kwa kusema kwamba tatizo hilo ni sugu kwa wakazi wa vingunguti na maeneo ya karibu na vingunguti  na wote wanao tumia njia hiyo kwa usafiri.
Mwisho bwana Isihaka  alimalizia kwa kuiomba serikali na mamlaka husika  kulitafutia ufumbuzi swala ili hilo kuwaepusha au kuwaondolea kero hiyo inayo wakabili katika nyanja  muhimu ya usafiri ikiwa ni pamoja na kuziba baadhi ya mashimo yaliyopo katka barabara hyo inayofahamika kama kwa buguruni mnyamani.


Mpaka habari hii inachapishwa jitihada za mwandishi wetu za kukutana na kufanya mahojiano na uongozi  wa eneo hilo azikuzaa matunda kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu.
Na msafiri mohamedi

No comments:

Post a Comment