Thursday 27 October 2016

YOSEFO YAANZISHA MFUMO WA PAMOJA KWA WAKULIMA



NA SALOME MWASAMALE, DAR
KATIKA kukabiliana na changamoto ya soko kwa wakulima wadogo wadogo benk ya Yetu microfinance kwa kushirikiana na kampuni ya vijana ya kitanzania ya Green Terk na shirika la YOSEFO wameanzisha mfumo wa kilimo cha pamoja (farm park) ili kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo hapa nchini.

Akizungumza kwenye semina ya wakulima wadogo kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini iliyofanyika jana jijini Dar es salaam mkurugenzi mtendaji wa Yetu microfinance Bank Altemius Millinga alisema mpaka sasa wakulima wadogo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa masoko kutokana na kila mmoja kulima pekee yake.

“Dhana iliyopo hapa nchini ya wakulima wadogo kila mmoja kulima pekee yake katika maeneo tofauti ndiyo inayosababisha wakulima kushindwa kuzalisha kiasi cha kutosha hivyo kusababisha ugumu wa upatikanaji wa soko” alisema Millinga.

Kufuatia hali hiyo alisema ndiyo maana Yetu Microfinance Bank wameamua kuanzisha mfumo wa kilimo cha pamoja (Farm Park) ili kuondokana na changamoto hiyo ambayo imekuwa sugu kwa wakulima wadogo hapa nchini.

Katika mafunzo hayo wakulima hao wamefundishwa namna ya kulima kilimo cha kisasa chenye tija cha Green House na kile cha umwagiliaji kwa njia ya matone ili kupata mafanikio kutokana na kazi hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa semina hiyo mkulima Meinrad Lupenza alisisitiza kuwa wakulima wadogo wanania ya dhati ya kujiletea maendeleo hivyo waliiomba Yetu Microfinance Bank kuharakisha zoezi hilo.

Kilimo cha “green house” eneo lenye upana wa mita 8 na urefu wa mita 15 aka kukamilika linaandaliwa kwa gharama ya shilingi milioni 7.5 na linadumu kwa muda wa miaka mitano hadi kumi lakini baada ya mavuno linaingiza faida ya kuanzia milioni 50-80.
 
 Mkurugenzi mtendaji wa Yetu Microfinance Bank Altemius Millinga akipanda mti kama ishara ya uzinduzi wa uanzishwaji wa kilimo cha pamoja (Farm park) picha na Salome Mwasamale.





No comments:

Post a Comment