Thursday 27 October 2016

SUNRISE WAIDI KUSHRIKIANA NA TSJ.



Na Sabore Laizer

Kituo cha radio cha Sunrise kilichopi mkoani Arusha kimeahidi kutoa ajira kwa mwanafunzi wa chuo cha Time School of journalism pindi wakimaliza masomo kwa ngazi  ya astashada na stahada .

Akiongea na mwanafunzi mkuu wa idara ya rasilimali watu mapema wiki hii wakati wa ziara ya kimasoma bwana Wolter kileo alisema radio inampago wa kuongeza nguvu kazi ili waweze kukidhi matakwa ya taasisi .


Vile vile bwana kileo alitoa nafasi  kwa mwanafunzi wa uwandani kwa ngazi ya astashada na stashada na kuahidi kuwa watapata ushirikiano pindi watakapo kuwa katika mazoezi kwa vitendo "alitoa rai kwa mwanafunzi wajitume katika masomo kwani wakijitahidi itakuwa rahisi kwao wakati wa mazoezi" alisema bwana kileo.

Naye Mratibu wa masomo katika chuo cha Time school of Journalism Bi Blandina Semaganga alishukuru uongozi wa sunrise radio kwa utayari na ushirikiano walionesha kwa chuo wakati wa ziara ya kimasomo mkoani Arusha.

Pia Bi Semaganga aliwahakikishia uongozi wa sunrise kuwa chuo kinafundisha vizuri hivyo wategemee kupata wanahabari wenye kiu kuhabarisha umma Bi Semaganga aliongeza kuwa chuo kinafundisha uadishi wa habari kwa nyanja sote yaani radio,televisheni,magazeti na  uandishi wa mtandaoni.

Baadhi ya mwanafunzi walishukuru wa serikali ya mwanafunzi na uongozi wa chuo kwa kufanikisha ziara ya kimasomo katika mkoa wa Arusha kwani imewasaidia wao kujua fursa mbalimbali ,waliofanikiwa kuomba nafasi za uwandani ni Odriani Masawe na Ireni mboya.

 

No comments:

Post a Comment