Friday 28 October 2016

SERIKALI YALALAMIKIWA JUU YA UPANDISHWAJI WA KODI



NA SALEH JUMA

Wafanyabiashara wa   soko dogo    lililopo kinondoni manyanya wamelalamika juu ya kukosekana kwa wateja  na biashara  kuwa mbaya kutokana na kupandishiwa kodi na bidhaa kuuza kwa bei yajuu.
Ndugu Saidi Abdallah ambaye ni mfanyabiashara wa vifaa vya simu katika soko hilo alisema kuna upungufu mkubwa wa wateja katika biashara yao ambayo tofauti na mwaka mmoja nyuma.
 
“Mwaka jana na mwaka huu biashara iko tofauti kabisa kwani unaweza kufungua duka tokea asubuhi mpaka saa saba bado hajapita mteja kodi imepanda halafu pia bidhaa huko tunapo nunua kwa jumla bei ipo juu na sisi tunapo uza wateja wanalalamika”

Aidha kwa wafanyabiashara wa vyombo vya plastic nao wamesema kwa upande  wao biashara ni ngumu kwani ushuru wa kuingiza vyombo ni mkubwa kwa hivyo mpaka inafika kuuzwa chombo dukani kwa bei yake inakua ipo juu kidogo hivyo wateja wengi wamekua hawaonekani mara kwa mara kujipatia mahitaji yao.
 
Kwa upande wa wafanyabiashara wa vyakula kama vile ndizi,mihogo,na viazi wamesema kwa upande wao kidogo biashara imekua afadhali nzuri kwani wateja hufika mara kwa mara kununua bidhaa kwaajili ya chakula kwani kula ni muhimu kwa mwandamu hivyo hakuna sababu inayomfanya  mwanadamu kushindwa kula hata kama maisha yapo juu.
 
Lakini pia wameiomba serikali kupunguza kodi kwa wafanyabiashara ili waweze kujimudu kimaisha kwani wengi wa wafanyabiashara ni wanafamilia na zinawategemea na biashara ndio kila kitu kwao wanazo zitegema ili kumudu maisha yao.

No comments:

Post a Comment