Friday 28 October 2016

Yanga yaitisha Mbao



Husna Kyelula
Baada ya kuwasambalatisha Kagera Sugar katika uwanja wa Kaitaba kwa mabao 6-2, na kuwamalizia kipigi hiko maafande wa JKT Ruvu kwa mabao 4-0, na kutimiza jumla ya mabao 10, katika mechi mbili.
Image result for yanga sports club
Yanga baada ya kuwa na rekodi hiyo kubwa ya magoli imewatisha wapinzani wao Mbao ambao wanakwenda kukutana nao siku ya jumapili katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Mboa Athanas Machael alisema kuwa hawaogopi rekodi hiyo ambayo Yanga wameiweka na wanakwenda kushindana na kutaka pointi tatu muhimu kwa mabingwa hao watetezi.
 Image result for yanga sports club
“Yanga ni timu kubwa kuliko timu yetu na tunatambua kuwa ndio mabingwa watetezi lakini hatuogopi kuwa waliweza kushinda jumla ya magoli 10, katika mechi zao mbili zilizopita”alisema
Pia napenda kuwaambia wapenzi na mashabiki wa Mbao wakae mkao wa kula na waamini kuwa tunakwenda kuchukua pointi tatu muhimu dhidi ya mabingwa hao watetezi wa ligi kuu bara.
Image result for yanga sports club





1 comment:

  1. Safi sana Dada Husna unajua na umeandika vitu vizuri.

    ReplyDelete