Tuesday 25 October 2016

Bei ya chakula yazua gumzo ziara ya masomo Mkoani Arusha.

Na Alfredy Geoffrey Mhagama.

    Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Time school of journalism (Tsj) kilichopo jijini Dar es salaam wamekuwa na maoni tofauti tofauti kuhusiana na bei ya vyakula katika ziara yao ya kuelekea  Arusha kufatia beiya vyakula kuwa juu.


[Baadhi wa wanafunzi wa chuo cha Times school of journalism wakiwa wanaelekea hotelini kununua chakula]


    Wakizungumza na mwandishi wetu kwa nyakati tofauti tofautiwanafunzi hao wameeleza kuwa walipelekwa kula sehemu ambayo bei ya chakula ipo juu ambapo sahani ya chakula in elfu 3,000hadi elfu 7,000 na kupelekea wanafunzi kutumia pesa nyingi kwa ajili ya chakula wakiwa njiani korongwe Mkoani Tanga kuelekea  Mkoani Arusha.

    Abeli Charles mwanafunzi wa Diploma ya nne  katika chuo cha Tsj alisema kuwa wameshangazwa na kitendo cha viongozi na walimu kuwapeleka katika hoteli  za gharama ambapo chipsi kavu ni  3,000 hadi  7,000 hali iliyopelekea kuaribu bajeti yake  na mwanafunzi wengine kutokana na fedha walizopewa in kwa ajili ya Siku zote katika ziara yao ya masomo Mkoani  Arusha.

   Pia Maria kilua mwanafunzi wa Tsj  Diploma ya pili naye alisema kuwa being ya chakula ilikuwa juu  licha ya baadhi ya wanafunzi kwa upande wao ilikuwa kawaida kutokana na bajeti yao japo kuwa wengi wao waliona being ilikuwa kubwa tofauti na walivyokuwa wakitegemea licha ya viongozi kuahidi kuwapeleka sehemu ambayo chakula kitakuwa bei ya kawaida ila haikuwa hivyo.

[Baadhi ya wanafunzi wa Tsj wakinunua chakula katika hoteli ya kilimanjaro wilayani Korongwe Mkoani Tanga]

   Licha ya wanafunzi kulalamikia bei ya chakula baadhi ya wanafunzi kwa upande wao ilikuwatofauti,Erick Kavishe mwanafunzi wa Tsj  BBC first alisema kuwa kwa watu wanaotoka Mikoa ya kaskazini kununua chakula 3,000 hadi 7,000 katika hoteli  mbalimbali ni kawaida ila kwa watu wa Mikoa mingine kama Dar Es Salaam kwao na kitu cha tofauti.
[Wanafunzi wakipata chakula katika hoteliya kilimanjaro iliyopo Mkoani Tanga]


  Kwa upande wake walimu wa chuo hicho cha Tsj Bwana George alisema kuwa walilazimika kwenda kula katika hoteli  hiyo kutokana na kuvurugika kwa ratiba na pia wanafunzi kwa muda huo walitakiwa kupata chakula na kuahidi kuwa watajitaidi kutafuta sehemu ambayo itakuwa na bei za kawaida za chakula.



  Pia Rais wa chuo cha Time School of journalism (Tsj) Sabore Laizer  naye alisema kuwa walilazimika kuwapeleka katika hoteli hiyo kula kutokana na mwingiliano wa ratiba na vilevile hoteli  hiyo ni sehemu ambayo mabasi mengi yanapitia hapo na abiria kupata chakula hivyo hawakutegemea kukuta  bei za vyakula  kama zitakuwa juu na kuahidi kutatua changamoto hiyo.

No comments:

Post a Comment