Thursday 27 October 2016

SERIKALIYATAKIWAKUUNDA SERA KWA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI






NA SALOME MWASAMALE,Dar
SERIKALI imetakiwa kuunda sera maalum kwaajili ya watu wenye ulemavu wa akili (vichaa, wendawazimu) ili kukabiliana na unyanyapaa na unyanyasaji dhidi ya kundi hili lililosahaulika.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es salaam na mkurugenzimtendaji wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Focus in Solution Group (FSG) Mohamed Mchingama alipokuwa akizungumza na jambo leo kuhusiana na kukithiri kwa vitendo vya unyanyapa na unyanyasaji miongoni mwa jamii dhidi ya kundi hili maalum.

Mchingama alisema kundi hili limeshaulika kabisa katika jamii lakini chakushangaza hata serikali imelitenga kundi hili ambalo pia linahitaji msaada wa hali ya juu.

"Watanzania tunajipanga kukabiliana na magonjwa mbalimbali kama vile kisukari, kansa, Tb, upungufu wa damu lakini wakati mwingine tunajiandaa hata kukabiliana na vifo tunasahau kabisa kukabiliana na ulemavu wa akili (ukichaa na uwendawazimu) na kusahau kuwa huu ni ugonjwa kama magonjwa mengine na yanaweza kumkuta mtu yeyote katika maisha", alisema Mchingama

Kwa upande wake mtafiti wa haki za binadamu katika kituo cha sheria na haki za binadamu (LRHC) Fundikila Wazambi alikiri kusahaulika kwa kundi hili na kuongeza kuwa hata yeye na taasisi yake hawajawahi kufanya utafiti kuhusu kundi hili.

“Ni kweli kuwa kundi hili limesahulika serikali inapaswa kuandaa sera mahususi kwaajili ya kundi hili ili liweze kutizamwa kwa jicho la tatu na kuangalia namna ya kulinusuru kwa kuwa unyanyapaa na unyanyasaji dhidi yao umekuwa ukiendelea siku hadi siku”, alisisitiza Wazambi. 



Diwani kata ya Kunduchi Michael Urio akipokea cheti cha heshima kwaajili ya kuwahudumia watu wenye ulemavu wa akili.Picha na Salome Mwasamale,Dar
 


No comments:

Post a Comment