Wednesday 26 October 2016

MSAAD A WA TSJ WANUFAISHA LAIBONI

Na Fatuma Sultani


 Chuo cha uandishi wa habari tsj kilichopo jijini dare s salaam kimetoa msaada katika shule ya msingi laiboni walipokuwa kwenye ziara yao ya kimasomo mkoani ARUSHA.Hiyo ilitokana na wanafunzi hao kuguswa na hali halisi iliyopo shuleni hapo.


Shule hiyo ambayo kihistoria ilianzishwa na mzee wa kimasai LAIBONI mwaka 1997 wilayani Monduli kutokana na tatizo lililompata la kufiwa na mtoto wake kwa ajali ya gari,hivyo kumpelekea mzee huyo kuamua kuanzisha shule yake mwenyewe ya LAIBONI.

Wanafunzi wa chuo hicho walitoa msaada wa madaftari,peni,penseli,sabuni na vingine vingi kwa wanafunzi wasomao shuleni hapo kwani walikuwa wanawasaidia wanafunzi hao kuweza kuepuka changamoto ndogondogo zitakazowakumba shuleni hapo.
    


Akiongea na chombo chetu cha habari mratibu wa masomo wa tsj Bi BLANDINA SEMAGANGA alisema kuwa wanajisikia faraja sana kutoa msaada shuleni hapo pia anawapongeza wanafunzi kwa kuwa na moyo wa  utoaji kuwasaidia wanafunzi wenzao pindi wapatapo matatizo,na pia wanajenga uhusiano mzuri na watu wanaowazunguka kwenye jamii.


.Walimu mkuu wa shule hiyo Bi.ROGAT MBUYA alisema anashukuru kupata msaada huo kwani ni kitu cha kiungwana sana,na anaiomba serikali pamoja na jamii ijaribu kuangalia shule hiyo kwa jicho la tatu kwani wanaupungufu wa madarasa na walimu wanaomba waongeze na mengine mengi
.

Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliimba na wimbo wa taifa TANZANIA  na kumalizia na wimbo wao wa shule wa LAIBONI LAIBONI

No comments:

Post a Comment