Wednesday 26 October 2016

SHULE YA MSINGI LAIBONI

     Na Shinuna

Laiboni ni shule ya msingi inayopatikana wilaya ya Monduli mkoani Arusha.Shule hii ina historia ya kipekee nchini Tanzania tofauti na shule nyingine.ni moja ya vivutio mkoani hapo.
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari TSJ waliweza kupata nafasi ya kutembelea shule hiyo ikiwa ni moja ya maeneo ya ziara zao za kimasomo mwezi wa 10.


Akiongea na mwandishi wetu Makamu wa rais bi Fatma Sultan alieleza kuwa "nia na madhumuni ya kutembelea shule hii ni kujua vitu vingi kutokana na chanzo cha kuwepo kwa shule hii kusisimua watu wengi"

Aidha mwalimu mkuu wa shule hiyo kushirikiana na walimu wengne weliweza kuwapokea wanafunzi hao vizuri na kuweza kutoa historia ya shule hiyo kwa ufupi.Mwl.mkuu wa shule hiyo bi Rogati Mbuya alielezea kuwa shule ya msingi Laiboni ilianzishwa na juhudi za mtu mmoja ambae ni mganga wa jadi kimaasai anaitwa"laiboni"ila majina yake halisi ni Meshuko Mapii ambae aliweza jenga shule hii mnamo mwaka 1997 kwa madhumuni ya kuepusha ajali baada ya mtoto wake kugongwa na gari akielekea shule ya msingi Eslaley ilyoko ng'ambo ya barabara.

Vile vile pamoja na kutolewa elimu katika shule hiyo kuna changamoto nyingi wanazo kutana nazo walimu pamoja na wanafunzi hao ikiwemo chakula, maji na kubwa zaidi ni uchache wa madarasa kwani mpka hivi sasa wanafunzi wa awali wanasoma nje.



Hata hivyo alieleza kuwa pamoja na changamoto hizo hawajashindwa kuendelea kutoa mafunzo na kujitahidi kuwafundisha kadri iwezavyo huku akiendelea kujibi maswali ya wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari time school of journalism, wanachuo wengne walipata fursa ya kucheza na kuchanganyika na wanafunzi wa Laiboni.


Wanachuo hao wa chuo cha uandishi wa habari TSJ wakiongozana na mkurugenzi wao wa masomo Bi Blandina Semaganga pamoja na Mlezi wao George Baltaza hawakwenda mikono mitupu waliweza kutoa baadhi ya mahitaji kama sabuni, madaftari na kalamu.

No comments:

Post a Comment