Thursday 27 October 2016

WATANZANIA WAHIMIZWA KUKUZA UTALII WA NDANI



NA SABORE LAIZER
Watanzania wakumbushwa kukuza Utalii wa ndani ili waweze kuvitangaza vivutio vilivyomo nchini kwa Watalii kutoka nje, alisema Bwana Johaness Japheth   katika mamlaka ya ngorongoro  akiongea na Wanafunzi wa chuo cha Time school of Journalism cha jijini Dar es salaam .
(muongozaji wa hifadhi ya ngorongoro bwn johanes akiongea na wanafunzi wa tsj)


Bwana Japhet aliongeza kwamba wanapokea wageni wengi kutoka nje ya nchi, mwamko ni ndogo sana kwa wazawa  hii inachangia watanzania kushindwa kutangaza vivutio vilivyomo nchini.
Naye afisa utalii wa mamlaka hiyo ndugu Moinga lesasi alisema kuwa viingilio vinafikika kwa kila mtanzania  kwa watoto kuanzia miaka mitano  mpaka kumi na saba ni shilingi 2600 na mtu
mzima ni 11800 hii ni baada ya mwaka wa fedha kuanza yaani 2016/2017 .
                

  (Wanafunzi wa TSJ wakielekea ndani ya kreta ya Ngorongoro
Pia aliongeza kuwa kuna gari maalumu kwa watanzania kuingia kreta ya ngorongoro kwa kuchangia mafuta lita mia moja ili kurahisisha kufanya mzunguko  (game drive).
Wanafunzi wa chuo cha Time school of Journalism walionekana kufurahia ziara hiyo ya masomo baada ya kumaliza Mizunguko  ndani ya kreta ya ngorongoro waliendelea kuuliza maswali kwa mwongozaji bwana Johaness wakitaka kujua utofauti za nyakati za masika na kiangazi kwa watalii



                  (Baadhi ya vivutio vinavyopatikana ndani ya Ngorongoro)
Hifadhi ya ngorongoro ni ya kipekee duniani kutokana na vivutio vilivyomo, watalii wanaingia kila kila siku na wengine hupenda kufanya sehemu ya kimasomo hivyo tunapokea taasisi nyingi za elimu

No comments:

Post a Comment