Thursday 27 October 2016

NDALICHAKO AVURUGA UCHAGUZI WA MEYA UBUNGO



Na Christian John
Baada ya mchakato wa muda mrefu wa kumtafuta Meya wa Wilaya mpya ya Ubungo kufikia tamati katika hali ya kushangaza  madiwani toka chama cha CHADEMA wamesusia uchaguzi huo.
Aidha uchaguzi huo uligubikwa na wingu zito mara baada ya waandishi wa habari kuzuiwa kuingia katika ukumbi wa uchaguzi jambo lililoleta mkanganyiko kwa wananchi kwa kukosa habari muhimu ambazo ni haki yao.
Akizungumza kwa hisia kali Mh.Diwani wa Mbezi Beach Florence Lupomo amesema kuwa walikuwa ukumbini hapo kutoa sapoti kwa madiwani wenzao ili kuhakikisha UKAWA inamiliki jiji lakini kwa kile alichokiita hujuma za CCM kuwarudisha nyuma kwa kufanya maamuzi ya ajabu.
“Huu ni uhuni aisee Ndalichako amefuata nini huku yeye yupo Ilala ameapa huko kama diwani huku hatumjui sisi,inauma sana kuona tunaonewa ila hatukubali kabisa”
Kwa upande wa Chama cha mapinduzi wao waliendelea na uchaguzi huo huku mtoto wa aliyekuwa spika wa Bunge Samuel Sitta,Benjamin Sitta akiibuka kidedea wa uchaguzi huo.
Chama cha Chadema kimetoa tamko na kusema kitapeleka suala hilo mahakamani.



No comments:

Post a Comment