Wednesday 26 October 2016

Bei ya nyanya yapolomoka soko la Buguruni.

Na Alfredy Geofrey Mhagama

   Wafanyabiashara wa soko la Buguruni ililopo katika Wilaya ya Ilala jijini Dar Es Salaam wamelalamika baada ya bei ya nyanya kushuka na kupelekea kupata hasara huku wanunuzi kwa upande wao ikiwa ni furaha.

   Wafanyabiashara hao wameeleza kuwa  Mkoa wa Dar Es Saalaam unategemea nyanya kutoka nje ya mkoa  hivyo inawalazimu wao kununua kwa bei ya juu na kuuza kwa bei ya hasara ambapo tenga uuzwa kwa sh 52,000 hadi kufikia sh 40,000.


   Akizungumza na mwandishi wetu mfanyabiashara Juliana Kimaya alisema "Biashara ya nyanya sasa imekuwa hasara kutokana wakulima kuunza kwa bei ya juu kwa wafanyabiashara huku bei ya sokoni ni dogo na endapo utapandisha bei nyanya zinakuozea"

                             
   Pia Shabani Njore alisema kuwa bei ya nyanya imeshuka kwa sasa pia hata wateja ni wachache sana na nyanya ni nyingi sokoni hali inayopelekea nyanya kuozea sokoni na kupata hasara au kuuza tu kwa bei ya chini ili kuebusha hasara kubwa.

   Kwa upande wa wateja sokoni hapo wamesema kwa sasa bei ya nyanya ni ya kawaida ambayo kila mtu anaweza kununua kuliko hapo mwanzoni ambapo bei ilikuwa juu sana .


   Aidha kwa wafanyabiashara wa nyanya sokoni hapo wameiomba serikali kuwajengea kiwanda cha kusindika mazao ya mbogambaga ili kuondoa hasara wanayoipata kutokana kushuka kwa bei ya nyanya na kukosa wateja pia kwa wingi na kupelekea nyanya kuoza zikiwa sokoni. 
                            

No comments:

Post a Comment