Wednesday 26 October 2016

LIPULI MPIRA MWINGI ILA WAMEAMBULIA KICHAPO

Na Fadhili Kijanjali

Club ya mpira ya Iringa inayokipiga ligi daraja la kwanza maarufu kama Lipuli jana imeambulia kichapo cha bao3 kwa0 kutoka kwa Friends Ranges yenye makazi yake jijini  Dar es salaam katika mechi za mizunguko zinazoendelea. 
Kikosi cha Lipuli kabla ya mchezo kuanza hapo juzi uwanja wa karume jijini Dar es salaam


Club ya Lipuli ilianza kwa kasi mchezo huo huku ikionekana kuwazidi uwezo Friends Ranges na kumiliki mpira kwa kiasi kikubwa sana katika dakika za mwanzo nakuonyesha wazi kuwa wanaweza kuushinda mchezo huo.  
Vijana wa Friends Ranges wakisali kwa pamoja kabla ya mechi yao dhidi ya Lipuli uwanja wa karume jijini Dar es Salaam



Baada ya dk15 za mchezo huo club ya Friends Ranges ilijiandikia bao la kwanza kupitia kwa mchezaji wao Almasi Mkinda aliyevalia mgongoni jezi namba 19 bao lililowafanya lipuli kuzidiwa kwa kiasi kikubwa baada ya bao hilo.


Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika lipuli walikuwa nyuma kwa bao1 huku Friends Ranges wakiongoza    



Kipindi cha pili kilianza kwa pande zote mbili kutoshana nguvu na dk ya 68 Friends Ranges wakajiandikia bao lao la pili kupitia kwa Fred Cosmas aliyevalia jezi no3 mgongoni nakuwafanya Lipuli kupoteza mwelekeo wa mchezo huo.  
Kocha wa Friends Ranges Edward Christopher akizungumza na wachezaji wake wakati wa mchezo dhidi ya lipuli uwanja wa karume jijini Dar es salaam


Khali hiyo iliwafanya Lipuli kupotea kabisa kabisa mpaka dk90 za mchezo huo, na ndani ya dk4 za nyongeza Rangers wakajiandikia bao lao la tatu kupitia kwa mchezaji wao Isihaka nakufanya mchezo huo umalizike kwa Lipuli kuambulia kichapo cha bao3.  
Wachezaji wa Friends wakishangilia bao lao walilolipata katika dakika za nyongeza kupitia kwa mchezaji wako Isihaka uwanja wa karume jijini Dar es salaam
 



Kwa upande wake kocha wa Friends Ranges Salvatory Edward amesema lipuli kucheza mpira mwingi haikuwa kigezo cha yeye kukosa ushindi kwakuwa aliamin vijana wake wana mbinu nyingi za ufungaji.



No comments:

Post a Comment