Wednesday 26 October 2016

Usafi washamili soko la Buguruni.

Na Peter Mhina

  Hali ya usafi  ya soko la buguruni  yaimarika baada ya halmashauri  ya manispaa ya ilala kusimamia kikamilifu  zoezi la usafi  katika soko hilo. Baada  ya kuweka watu  maarumu ambao wanahakikiasha  hakuna taka zinazo zagaa ovyo katika mazingira wanayo fanyia biashara.

 Mwanzoni soko hilo  lilionekana   kama  halina usimamizi mzuri baada  ya kuwepo taka kila eneo  na maji machafu yanayotuwama hususani  wakati  wa mvua nyingi,na kusababisha harufu mbaya katika eneo hilo la soko.


  MOHAMED ULONGO ni mfanya biashara alisema " tunaishukuru  serikali kwa kijumla kwa kuzingatia usalama wa raia na mali zao hasa katika soko letu hili la buguruni na sasa kumekuwa na hali nzuri katika maeneo yetu ya kazi  kumesaidia kuepukana na magonjwa ya milipuko hasa kuptia biashara tunayo ifanya katika shughuli zetu za kilasiku katika kuzalisha kipato".

  Hivyo nachukua nafasi hii pia kuwa hamasisha  wafanya biashara wenzangu kufanya usafi katika maeneo yetu  ya kazi hasa katika maeneo  yetu  kuepukana na magonjwa ya milipuko


  Hata hivyo wafanyakazi hao wameishauri serikali katika kuhamasisha wananchi wanaofanya kazi katika mazingira yenye mkusanyiko wa kazi katika masoko .,na vituo vya daladala kuweza kutunza mazingira,
                               

No comments:

Post a Comment