Friday 28 October 2016

Simba hii, siyo ya mchezo

  Husna Kyelula
Aliyekuwa kocha wa Yanga Hans Plujim ambaye alishindwana na timu hiyo na kuamua kuachana na timu hiyo ambayo ilionekana kama kutoaanza vizuri msimu huu chini ya Hans
Image result for simba sports club
Baada ya makubalaino ya Hans na Yanga ndio kocha huyo alisema kuwa Yanga wanakazi kubwa sana ya kufanya msimu huu kwani wapinzani wao Simba siyo wa mchezo mchezo.
Hans ambaye alizungumza na gazeti hili wiki moja iliyopita alisema kuwa anawatakia kila la heri timu yake ya zamani Yanga lakini wanakazi kubwa ya kufanya ili kuwazidi wapinzani wao Simba
‘’ Simba msimu huu wamejipanga sana na nataka kuwaambia kitu tena kwa kuwakumbusha wapenzi, mashabiki, wachezaji na viongozi kwa ujumla wanakazi kubwa ya kufanya ili kuweza kulitetea taji lao ambalo walilinyakua msimu uliopita’’alisema Hans
Image result for simba sports club
‘’Siyo kama nawatisha ila nimeiona Simba kuwa wapo vizuri na wanania ya dhati kuona wanakuwa mabingwa msimu huu kwani hawataki mchezo mchezo kabisa katika kila mechi zao kama msimu uliopita huku wakiwa na kikosi bora tofauti na msimu uliopita’’alisema
Hata hivi Simba watakuwa na kibarua kingine siku ya kesho katika uwanja wa Kambarage  kuwakabili Mwadui fc, ambao wanaangaika kupata matokeo msimu huu.
 Image result for simba sports club

No comments:

Post a Comment