Wednesday 26 October 2016

POLICE DAR NA ASHANTI UNITED ZATOSHANA NGUVU


Na Fadhili Kijanjali

DAR ES SALAAM
Katika mchezo wa kuendelea na mzunguko wa ligi daraja la kwanza kwa mechi za kundi A hapo jana katika uwanja wa karume jijini dar es salaam timu ya Police Dar na Ashanti United jana zimetoshana nguvu kwa kutoka suruhu ya bao2 kwa2.
Kikosi cha Police Dar kabla ya mchezo kuanza katika uwanja wa karume jijini Dar es salaam


Police walikuwa wa kwanza kuandika gori katika mchezo huo dakika ya 40 kupita kwa mshambuliaji wao Hamadi Kambagwa bao lililowafanya police kumaliza kipindi cha kwanza wakiwa mbele kwa bao moja kwa bila.

Kipindi cha pili cha mchezo kilianza kwa kasi na Ashanti uonesha uwezo mkubwa nakuongeza mashambulizi hali iliyowafanya Ashanti kujipatia penalty dakika ya 75 iliyojazwa nyavuni na mshambuliji wa timu hiyo Yahaya Zaydi aliyevalia jezi nambari13.
Mshambuliji wa Ashanti United Yahaya Zaydi akitupia nyavumi mpira wa penalti uwanja wa karume jijini Dar es salaam


Dakika tano baadae Ashanti waliandika bao lakuongoza mchezo huo kupitia kwa mshambuliaji wao machachali Yahaya Zaydi aliyetupia bao hilo kwa kichwa Zaydi alionesha uwezo mkubwa katika mchezo nakuwasumbua walinzi wa Police Dar.
Wachezaji wa Ashanti United wakiomba dua kwa pamoja kabla ya mchezo kuanza kwenye uwanja wa karume jijini Dar es salaam


Dakika ya 86 ya mchezo huo mambo yalibadilika nakuwafanya walinzi wa Ashanti kukubali suruhu baada ya mshambuliaji wa Police Evance Alfred kuandika bao lakusawazisha lilifanya mchezo kumalizi kwa sare ya bao 2 kwa 2.

Kwa upande wa makocha wa timu zote mbili wamelalamikia uwezo mdogo wa waamuzi unaoneshwa na waamuzi wanachezesha michezo ya ligi daraja la kwanza nakuongeza kuwa waamuzi hao huchangia michezo kuwa migumu.
Waamuzi wa mchezo kati ya Police Dar na Ashanti United wakizungumza kabla ya mchezo huo kuanza uwanja wa karume jijini Dar es salaam

No comments:

Post a Comment