Thursday 27 October 2016

MAZINGIRA YA SOKO LA BUGURUNI KERO KWA WANANCHI WA KARIBU



Na fadhila mohamed

      Kutokana na mazingira ya soko la buguruni lilulopo katika manispaa ya wilaya ya ilala jijini dar es salaam     kutokuwa katika hali ya usafi ni kero kwa wananchi wa karibu  kutokana na mrundikano wa maji machafu yanayokusanyika wakati wa mvua




sehemu  ya mbela sokoni hapo ambapo magari hupakiwa


.
      Mmoja wa wakazi wa eneo hilo la karibu anaejulikana kama juma  mzaramo  alieleza kuwa miundombinu ya kupitisha maji taka  sokoni hapo ni mibovu kwa kiasi kikubwa kwani husababisha maji kutapakaa kila eneo na hatimaye huoza na kuanza kunuka .

      Licha ya wakazi hao kulalamika lakini pia baadhi ya wateja na wafanyabiashara sokoni  hapo wanakerwa na kitendo hicho ambacho kinasababisha hali ya hewa kuwa mbaya baadhi ya maeneo kuzunguka soko hilo.





Hii ni moja sehemu ya nyuma sokoni hapo ambayo maji  hutuama wakati wa mvua


          Kwa upande wake mwenyekiti wa soko hilo yeye alithibitisha kuwepo kwa kero nyingi sokoni hapo na kuwaomba wakazi wa karibu kuthibiti babadhi ya watu wanaokuja kutupa taka sokoni na kushirikiana katika kulinda usafi .
 
         Aliendelea kusema kuwa matatizo haya yanajulikana na manispaa na yapo katika ripoti ya utekelezaji wa kero hizo.

No comments:

Post a Comment