Thursday 27 October 2016

Ziara ya Masomo yatoa ajira.



Ziara ya Masomo yatoa ajira.
Na Paulo Thomas.
Kufuatia ziara ya kimasomo ya chuo cha uandishi wa habari Time school of  Journalism  katika  Kampuni ya IPP Media upande wa uchapishaji wa gazeti la the Guardian iliyopo Mikocheni Dar es salaam imeibua fursa ya ajira katika Tasnia hiyo.
Akitoa utangulizi Ofisa  mahusiano  wa Kampuni hiyo ya IPP Media Anthony Mgeni alipokuwa anazungumza na wanafunzi hao wiki iliyopita alisema
“vijana wanatakiwa kutambua fursa za ajira hili kuweza kuondokana na changamoto za ajira hapa nchini”.
Hata hivyo alisema kuwa kujitambua pamoja na kujiamini  kunaweza kumfikisha mtu katika malengo na ndoto alizojiwekea kwa kuhakikisha kuwa ana amini juu ya kile anachokifanya.
Pia alitoa ufafanuzi juu ya namna wanavyotoa fursa mbalimbali  kwa wana tasnia  ya uandishi wa Habri na utangazaji ili kuweza kupata uzoefu wa tasnia hiyo na baadae kuweza kushinda na soko la ajira.
Baadhi ya wanafunzi katika ziara hiyo walitoa shukrani kwa uongozi wa Kampuni hiyo kwa fursa ambazo hutoa kwa wanafunzi kwa ajili ya kuwa na mazoezi ya vitendo ambayo huwajengea uzoefu wa kazi zao.
Hata hivyo mratibu wa masomo wa chuo cha Time School of Journalism Madam Blandina Semaganga alieyeongozana na wanafunzi hao alitoa shukrani za dhati kwa uongozi wa IPP Media  kwa kuwapa nafasi yakufanya ziara hapo.
Mbali na shukrani hizo Madam Semaganga aliahidi kutoa ushirikaino wa hali na mali  na uongozi wa kampuni hiyo ili kuweza kutumia fursa za wanafunzi kwenda kufanya mazoezi ya vitendo katika Media hiyo kwa ajili ya kupata fursa mbalimbali za ajira. 
Mhariri wa Gazeti la The Guardian Charles Mkude akizungumza na wanafunzi (hawapo pichani)katika ziara hiyo.
Msanii maarufu na mchora katuni Abdul Kingo akibadilishana mawazo na wanafunzi wa TSJ.
Mratibu wa masomo wa chuo cha Uandishi wa habari TSJ Bi.Blandina Semaganga akisikiliza maelezo toka kwa mhariri wa Gazeti la The Guardian (hayupo pichani) katika ziara ya

No comments:

Post a Comment