KITAIFA

   Na Alfredy Geofrey Mhagama
         
         Imeelezwa kuwa moja ya sababu ya kuanzishwa kwa shule ya msingi Laiboni iliyopo katika  kata ya Makuyuni Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha ni kufatia kifo cha moja ya mtoto wa mganga wa jadi  wa jamii ya kimasai aliyefahamika kwa jina la Meshuke Mapi kukongwa na gari alipokuwa akielekea shule ya msingi Eslaley.
    

[Shule ya msingi Laiboni iliyopo wilwyani Monduli Mkoani Arusha iliyoanzishwa mwaka 1997]

 Hayo yalielezwa na mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya msingi Laiboni Bi Rogatha Mbuyaalipokuwa akizungumza na wanafunzi wa chuo cha Times school of jounalism kilichopo jijini Dar Es Salaam.
       
[Walimu Mkuu wa Shule ya Msingi Laibon Bi Rogatha Mkuya akizungumza na waandishi wa habari

            Bi mbuya  aliongeza kuwa baada ya kifo cha mtoto wa mganga huyo wa jadi aliamua kuanzisha shule yake binafsi ili watoto wake na wajuu zake wote waweze kusoma hapo ambayo ilianza mwaka 1997 wanafunzi wakiwa wanasomea chini ya mbuyu.
      
      Pia bi Mkuya alisema kuwa shule hiyo ilipokuwa ikianzishwa watoto wa Mzee Meshuke ndio walikuwa walimu, alifanikiwa kujenga darasa moja pamoja na ofisi na baadaye shule hiyo ikasajiliwa na kuchukiliwa na serikali mwaka 2007 ambapo katika shule hiyo zaidi ya asilimia 90 ya wanafunzi ni watoto, wajukuu na vitukuu vya mzee huyo.
      
      Sanjari na hilo pia Mkuu huyo wa shule ya msingi Laiboni Bi Rogatha Mkuya aliweza kupokea msaada kutoka kwa wanafunzi pamoja na walimu wa chuo cha Times School of journalism [TSJ] ikiwemo Madaftari,kalamu,sabuni ya mche pamoja na sabuni ya unga box moja.

[Wanafunzi wa Times School of Journalism wakiwa wanaelekea katika Shule ya msingi Laiboni kutoa msaada]
     vilevile wanafunzi hao na walimu waliweza kuchangia kiasi cha pesa pia kutoka kwa kila wanafunzi kufatia bi Mkuya kueleza changamoto mbalimbali zinazokabili shule hiyo ikiwemo ukosefu wa maji wakati wa kiangazi hali inayopelekea wanafunzi kukosa chakula shuleni,pia upungufu wa madarasa mawili ya kufundishia.
[Rais wa Chuo cha Times school of journalism Sabore Laizer akimpatia mwanafunzi madaftari shuleni hapo]

No comments:

Post a Comment