Thursday 27 October 2016

WANAFUNZI WA LAIBONI WAHITAJI MSAADA



Na ANITHAN JAIL
 
Shule ya msingi Laiboni iliyoko mkoani Manyara wilaya ya Monduli imeanzishwa mwaka 1997 ikiwa na wanafunzi 9,mwanzilishi wa shule hiyo ni mganga wa kimasai.
 
Wanafunzi hao ni wajukuu na watoto wake ambao wanaishi kwenye familia au maboma tofauti.Darasa la saba mwaka wa kwanza walifaulu wanafunzi 12 na mwaka wa pili 19 bado mwaka huu alisema mkuu wa shule hiyo mwalimu Regeto Mbuya.

Kutokana na mganga huyo wa kimasai kupoteza binti yake aliamua kuanzisha shule iitwayo Islelai na sasa inaitwa Laiboni na serikali kuamua kumuunga mkono
Mwalimu Regeto alisema shule ina changamoto ya maji kwani wanategemea maji ya mvua na mabwawa,na chakula  kwani ardhi ya apo hairuhusu kupanda mazao yoyote
 
Pia wazazi wanachangia pesa ili watoto wao wapate chakula ambacho kinapikwa shuleni,na walimu wa shule hiyo hawajaanzisha miradi ya kuwezesha wanafunzi kupata chakula kwa haraka kwasababu ardhi ina mawe sana na wanyama pori kama tembo,fisi nk

Mratibu wa masomo Madamu Semaganga pamoja na wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari TSJ walifika shule apo wakiwa katika ziara ya kimasomo walichangai baadhi ya vitu kama sabuni,miswaki,madaftari.
 
Serikali na jamii kiujumla inabidi kuendelea kuunga mkono shule hiyo na kutoa misaada mbalibali kwani bado ina changamoto nyingi

No comments:

Post a Comment