ZA NDANI YA CHUO



MRUNDIKO WA TAKA WAZUA ZOGO TEMEKE.
Na Paulo Thomas 
 Wananchi wa wilaya ya temeke wameilalamikia serikali ya Mtaa kwa kuchelewa kupitisha gari la kubeba taka ambalo hupita kila baada ya wiki, akizungumza na gazeti la TSJ mkazi wa eneo hilo aliyefahamika kwa jina la Hassani Mohamed “alisema mtaa wao unaongoza kwa mazingira kuwa machafu kutokana na Serikali yao ya Mtaa kutofuatilia magari ya Taka na kutokuchukua taka kwa muda ambao umepangwa”.

 
Alisema swala hilo limekuwa ni kero kwa wakazi wa  eneo hilo kutokana na taka kukaa muda mrefu mitaani na kupelekea kutoa halufu kali na kushindwa kukaa kwa furaha, hata hivyo mwenyekiti wa Mtaa wa Temeke mwisho Ndugu Jafari Iddi “alisema wanashindwa kulifuatilia tatizo la usafi wa mazingira kutokana na Manispaa ya Temeke kudai kuwa hilo swala watalisimamia kwa muda halafu watawaachia viongozi wa Mtaa  na matokeo yake mpaka leo Serikali  ya Manispaa haitaki kuachia madaraka kwa viongozi wa Serikali ya Mtaa”.
Pia  mwenyekiti huyo aliongeza kuwa swala la magari kutokuchukua takataka  kwa wakati ni tatizo  la sehemu  ya kutupa takataka kuwa mbali, pia barabara kuwa na mashimo hivyo magari kushindwa kupita kwa urahisi.

No comments:

Post a Comment