Thursday 27 October 2016

WAFANYABIASHARA WA SOKO LA PUGU WALALAMIKA KUHUSU MIUNDOMBINU YA SOKO MIBOVU



Na:- Rahma Saidi
Wafanya biashara wa soko la Pugu Kigogo freshi wamelalamikia uongozi wa soko kuhusu suala la miundombinu kuwa mibovu na kusababisha biashara zao kuyumba kwa kiasi furani.
Wafanya biashara hao walisema kuwa kunatatizo la kutokuwepo na sehemu maalumu ya kujisaidi haja kubwa na ndogo (choo) na kusababisha baadhi ya wafanya biashara wengine kuacha kufanya biashara katika soko hilo.
Vilevile walisema kuna baadhi ya viongozi wanalipelekesha soko kidikteta zaidi kwa manufaa yao binafsi bila kujali haki za wafanya biashara hao.
Mmoja wa wafanya biashara Bwana Sudi Hassani alisema kuwa wamejalibu kushtaki katika uongozi wa soko hadi kwa diwani wa eneo hilo lakini bado hawakulifanyia kazi na kuona halina umuhimu kwao.
Bwana Sudi aliendelea kusema wanaumia na kuathilika hasa katika suala lakutokuwepo na sehemu ya kujisaidia yaani vyoo.
Hata hivyo mmoja wa viongozi Bwana Sospeter Mapanga alisema kuwa watalifanyia kazi suala hilo kwa haraka zaid.



No comments:

Post a Comment