Thursday 27 October 2016

SERIKALI IMEOMBWA KUREKEBISHA BARABARA YA KITUO CHA MAWASILIANO



Na Imani luoga

     Madereva wa mabasi jijini Dar es salaam wameiomba serikali kuboresha barabara ya kuelekea kituoni hapo ambayo huchangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa magari. 

Hii ni sehemu ya ndani ya kituo hicho cha mawasiliano ubungo



     Akizumgumza na mwandishi mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya kinondoni MUSSA NATTY amebainisha kuwa serikali inatambua tatizo la barabara hiyo na kuwa kwa kushirikiana na benki ya dunia wameandaa mradi ambao utahusika kuboresha miundo mbinu ya jiji la Dar es salaam.

      Kwa upande wao baadhi ya madereva wanaotumia kituo hicho wamesema kuwa ubovu wa barabara hiyo umekuwa na tatizo kwa kipindi kirefu sana na tangu  serikali iseme inatafutia ufumbuzi mpaka sasa hakuna kinachoendelea alisema Hussein juma mmoja wa madereva.

 

     Naye mmoja wa watumiaje wa barabara hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Bwn.Ally Mohamed mkazi  wa sinza alisema “tunapata tabu pindi tutumiapo barabara hii hasa wakati wa mvua kwani inajaa maji na kuwa na mashimo marefu’’alisema mkazi huyo




     Kituo cha mawasiliano kilifunguliwa mwezi October 2014 mara baada ya kuhamishwa kutoka katika eneo lililopo pembezoni mwa shirika la umeme Tanzania (TANNESCO).

No comments:

Post a Comment