Thursday 27 October 2016

WAFANYA BIASHARA WADOGOWADOGO WA SOKO LA BUGURUNI WALALAMIKA KULIPA USHURU MKUBWA



NA :- Rahma Saidi
Wafanyabiashara wadogowadogo wa soko la Buguruni jijini Dar es salaam walalmika kulipa ushuru mkubwa.
Akizungumza na gazeti la chipukizi leo mmoja wa wafanya biashara hao Bwana Ally Juma amesema kuwa ushuru wanaolipa ni mkubwa kuliko biashara wanazofany, ‘ushuru tunaolipa ni sh. 500 ukiangalia mzigo ulionunua wiki nzima haujaisha hivyo unapouza kila unalipa hadi mzigo uje kuishe faida inakuwa ndogo,’ alisema.
Aliendelea kusema kuwa anaiomba Almashauri ya soko hili liwasaidie katika suala hilo kwani pesa wanazopata ndizo zinawasaidia kukidhi mahitaji yao ya kila siku hivyo ipunguze ushuru huo walipe elfu moja kwa wiki kwani ukipiga hesabu miatano kila siku kwa wiki ni elfu tatu miatano.
Naye mtoza ushuru wa soko hilo aliyekataa kutaja jina lake alisema kuwa wafanyabiashara hao wanaonewa lakini sio kweli kwasababu ushuru huo ndio unasaidia mazingira ya soko hilo yawe na salama.
 Pia alisema kuwa  ushuru wanaolipa wafanya biashara hao ni mdogo, ‘kwasababu kuna wafanya usafi, magari ya taka, wazoa uchafu, na walinzi watalipwa na nani hivyo ushuru wanaotoa ndio tunawalipa watu hao’ alisema mtoza ushuru huo.
Haidha Halmashauri ya soko hilo ilisema kuwa wafanyabiashara wadogowadogo wote wamaeruhusiwa kufanya biashara zao na Mh. Rais hivyo hawatakiwi kusumbuliwa na walipe ushuru kulingana na mapato yao.



No comments:

Post a Comment