Thursday 27 October 2016

Takataka zawa kero


NA Daud Alex
Mwenyekiti wa mtaa wa Barabara ya mwinyi kata ya Kiburugwa wilaya ya Temeke JUMA ALLY NGONYANI  amepiga marufuku ya wakazi hao kutupa taka katika eneo ambalo amekataza kutupiwa taka kwani huo ni uchafuzi wa mazingira.
 
Akiuzungumza na SAFARI 255 kwanjia ya simu baada ya kamera ya safari 255 kuona taka hizo amesema kuwa tayari alikwisha kuwaambia wananchi hao kuwa wasitupe taka eneo hilo lakini hata yeye anashangazwa kuona wakizidi kutupa taka hizo.
 

Pia aliweka kamati ya ulinzi ili kuwazuia watu wanao tupa taka katika eneo hilo lakini inaonyesha kuwa wameshindwa kazi hiyo hivyo atavunja na kuunda upya kamati nyingine ili kuzuia hali hiyo kwani niya hatari kwa afya zao.
 
Baadhi ya wakazi walio karibu na eneo hilo wanasema kuwa hupatwa na harufu kali kutoka katika taka hizo hata wanapo jaribu kulinda watu wasitupe taka katika eneo  hilo huwa hawawaoni majira ya mchana bali hukuta taka hizo wanapoamka asubuhi.
 
Hata hivyo mwenyekiti wa mtaa huo amesema kuwa yeye na wajumbe wake wataweka sheria kali ikiwamo kila atakaye kamatwa akitupa taka katika eneo hilo atatoa faini ya shilingi elfu hamsini na kulisafisha eneo hilo,vilevile ameongeza kuwa uchafu huo uliopo watahakikisha jumamosi ijayo watafanya usafi kama agizo la mkuu wa mkoa wa Dar e s Salaam Poul Makonnda.
 

No comments:

Post a Comment