Friday 28 October 2016

WATANZANIA WASHAURIWA KUFUATA UZAZI WA MPANGO




NA SALEH JUMA

Watanzania washauriwa kufuata uzazi wa mpango na uzazi salama ili kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo la watoto wa mitaani linalotokana na wazazi kuto kumudu familia zao kwasababu  ya hali ngumu ya umasikini.

Hayo yamesemwa oktoba 25 na naibu waziri wa afya katika warsha ya siku mbili ya wadau mbalimbali wa sekta ya afya iliofanyika katika baraza la maaskofu kurasini jijini DAR ES SALAAM

“Wazazi na watanzania wenzangu tujitahidi kupanga uzazi salama ili kupunguza kabisa tatizo la watoto wa mitaani kutokana na ugumu wa maisha tunashindwa  kumudu familiazetu”

Aidha amewataka watanzania kujitokeza kupima virusi vya ukimwi ili kujua afya zao na kuanza tiba mapema endapo amegundulika kuwa tayari ameambukizwa virusi vinavyo sababisha ukimwi kwasababu serikali inatoa huduma hizo bure bila malipo yeyote.
 

No comments:

Post a Comment