Thursday 27 October 2016

MAJI MACHAFU KERO MALAPA

Tamriha Hamisi
Dar es salaam
 Wakazi wa mtaa wa malapa buguruni jijini Dar es salaam wamelalamikia baadhi ya nyumba zilizopo maeneo hayo kutiririsha maji machafu yanayotoka maliwatoni  (msalani yakiwa na harufu kali na watoto hucheza katika maeneo hayo bila ya kujua kuwa ni madhara kwao.




Waliyazungunza hayo na Safari 255 ilipotua kwenye maeneo hayo na kusema kuwa wanapata wakati mgumu sana kwa kuwa ni jambo llililodumu kwa muda mrefu bila ya kupata suluhisho la suala hilo.
Safari 255 ilijaribu kwenda serikali za mtaa wa malapa ili kupata taarifa juu ya suala  hili lakini hawakufanikiwa kukuta msemaji mkuu wa ofisi hiyo, na walipogeuka upande wa wamiliki halali wa nyumba hizo hawakuwa tayari kuongea chochote.

Pia wananchi hao waiomba serikali ya mtaa huo kuhakikisha inatilia mkazo na kulisimamia sula nhilo kwa nguvu na bidii zote ili kusaidia kulinda usalama wa afya zao na watoto wao wasio jua chochote.

Safari 255 limeahidi kufuatilia suala hili kwa bidii na kuhakikisha linapatiwa ufumbuzi na linakwisha kabisa katika mazingira yanayowazunguka wakazi wa eneo hilo, na kufanya jitihada na kumpa mwenyekiti wa eneo hilo.

No comments:

Post a Comment