Thursday 27 October 2016

KERO YA UKOSEKANAJI WA PARKING SOKONI BUGURUNI



               
 

Na Janeth frank
      Ukosefu wa sehemu ya kuhifadhi magari  yanaingia kuleta bidhaa na kununua bidhaa ndogondogo katika soko lililoko buguruni manispaa ya ilala jijini dar  es salaam ,imekuwa ni kero kubwa kwa wafanyabiashara wadogo wanakuja kununua bidhaa na wateja wa kawida.




      Baadhi ya wateja wanaoingia sokoni walieleza kuwa mara nyingi gari linapoingia au kutoka pande tofautitofauti za soko hilo watu hulazimika kusubiri gari lipite  ndipo watu waingie au kuwapisha makuli wanaokuwa wanatoa bidhaa ndani na kupeleka nje kitu mda mwingine unaweza ukasukumwa na kuanguka
.
       Lakini pia mmoja wa madereva wanaoingia kuleta bidhaa sokoni hapo alisema kuwa kitendo hiki kina tupa wakati mgumu sisi madaereva na akaotolea mfano ,kuwa sokoni mabibo kuna sehemu malum kwa ajili ya parking na kushusha mizigo sokoni hapo na akaiomba serikali iige mfano huo itakuwa vizuri sana.




       Kutokana na hali hiyo wafanyabiashara hao walitoa ombi  kwa serikali uongozi wa soko hilo kufanya utaratibu wa kutatua kero hiyo ya ukosefu wa parking.

No comments:

Post a Comment