Thursday 27 October 2016

WAFANYABIASHARA MACHINGA COMPLEX WAOMBA PUNGUZO LA KODI




Na imani luoga 

      Jengo la biashara maalumu kwa wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Machinga Complex lililopo katika wilaya ya ilala Jijini Dar es salaam tangu kukamilika kwake mwak 2013 limekuwa kivutio kikubwa kwa wafanyabiashara na wateja mbalimbali wanaotembelea soko hilo 
,
      Tangu kukamilika kwake changamoto mbalimbali zimejitokeza katika jengo hilo ikiwemo kuungua kwa jingo hilo, mgomo wa wafanyabiahsra kuhamia katika jingo hilo, lakini zaidi               Malalamiko kutoka kwa wafanyabiahsra mbalimbali wenye matatizo ya ulemavu wa aina mblimbali.

       Mwishoni mwa mwaka 2015 idadi kubwa ya walemavu waliweka mgomo kuitaka serikali iwapunguzie kodi pamoja nakuwapatia vizimba vya biashara maeneo ambayo yana muamko mkubwa wa biashara.

       Mwaka mmoja sasa umepita tangu mgomo ule upite, Chipukizi inaona haja yakufuatilia sakata hilo kwa kina nkuojua je limeisha kama serikali ilivyo ahidi au bado kuna changamoto zinaendelea kujitokeza.

      Salim Ahmud ni mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara wenye ulemavu ambaye yeye ni mlemavu wa ngozi “Sio kwa kiwango tulichohitaji” Anasema Salim, “ Serikali yetu ya mkoa inatekeleza ahadi kwa mwndo wa kinyonga sana, ingawa tunashukuru baadhi yetu wamefanikiwa kupata vizimba kariakoo lakini sisi wachche tuliobaki hapa tunakutana na changmoto mbalimbali, kwa watu wenye mattizo ya viungo n hasa miguu, jingo hili sio rafiki kabisa nawao”

      Machinga complex imejengwa kwa mtindo kwa ghorofa, kwa mujibu w Sali Anasema inawawia ngumu walemavu wa miguu na mikono kuweza kupanda juu kwa ajili ya biashara “ Hii sio tu kwa wafanyabiashara wenye ulemavu, bali hata kwa wateja wenye ulemavu ni ngumu kwa wao kupanda juu kununua au kuuza bidhaa 






       Anaeleza Salim huku akionesha muundo wa soko hilo, chipukizi linafanikiwa kuona vizimba vya biashara vilivyotengwa maalumu kwa ajili ya watu wenye ulemavu lakini vingi vinaonekana kufungwa kwa mujibu wa Salim anasema wamelazimika kufanya hivyo sababu ya ugumu wa biashara, mitaji midogo na changamoto z upatikanaji wa malighafi “wengi wanaoendelea na kazi hapa ni wale wenye ujuzi mbalimbali kama vile mafundi viatu na vifaa vya umeme, kwa sababu mitaji yao ni ujuzi wao”

     Halmashauri ya wilaya ya ilala ambayo ndiyo yenye dhamana ya jengo hilo wanakiri kutambua changamoto hizo lakini wakipinga suala la ugumu wa Biashara kwa mujibu wa mratibu wa biashara na maendeleo ya wnanchi ndugu Festo Maiko anasema tangu kufunguliwa kwa soko hilo wafanyabishara wamekuwa wazito kuhamia pale jambo linalochangia kuzorota kwa   

No comments:

Post a Comment