Friday 28 October 2016

Azam yashtuka!!


  Na.Husna Kyelula
Baada ta kutokuwa na muendelezo mzuri wa matokeo katika ligi kuu bara timu ya Azam kupitia kwa mtendaji wao mkuu Sady Kawemba alisema kuwa sasa wameshtuka.
 Image result for azam sports club
Kawemba alisema kuwa wameshatuka na kwa nini wamekuwa na muendelezo mbaya wa matokeo katika timu yao ambayo wameaanza nayo msimu huu chini ya kocha kutoka Hispania.
“Naweza kusema kuwa tumeshtuka kwanini tunakuwa na matokeo ambayo siyo ya kulizisha kwa mechi nyingi za ligi kuu bara ambalo tatizo hilo ni kwamba wachezaji wetu wametumika sana wamechoka”alisema
“Kwani ukiangalia wachezaji wetu wa kikosi cha kwanza wengi sana wametumika kwa muda mrefu bila ya kuwa na mapumziko ya kutosha huku wengine wakishindwa kabisa kuendelea na timu kwa kuwa wamepata majeraha ambayo yaliwawaka nje”alisema
“Kwa sababu hiyo tumeshtuka kuwa uchovu wa wachezaji ndio unaotufanya kupata matokeo haya mabayo kwa upande wetu siyo ya kulizisha lakini kwa kuwa tatizo tumeshalijua tinakwenda kulifanyia kazi”alisema
 Image result for azam sports club
Azam watakuwa na kibarua kingine kigumu siku ya kesho katika uwanja wa Kaitaba Bukoba kuwakabiri Kagera Sugar ambao nao wanaangaika kupata matokeo mazuri na wakiwa na kumbukumbu ya kupingwa mabao sita dhidi Yanga.
 Image result for azam sports club



1 comment: