Thursday 27 October 2016

WANANCHI WAFURAHISHWA NA KIVUKO BUGURUNI

Na Hamisa mkongo
Wakazi wa buguruni katika wilaya ya ilala jijini Dar es salaam wameipongeza hatua ya serikali ya kukamilisha kivuko cha daraja katika eneo la sheli kwani kumewasaidia kupunguza ajali za mara kwa mara zilizokua zikitokea katika eneo hilo

Akiongea na chipukizi mapema hii leo mmoja wa wakazi na watumizi wa kivuko hicho Albert Jumaalieleza furaha yake juu ya hatua ya serikali kusikiliza kilio chao cha mda mrefu “Naishukuru sana serikali yetu chini ya mheshimiwa rais John Maufuli kwa kuskiliza kilio chetu kwani tumekua tukitaabika sana wakati wa kuvuku huku magari yanapita” alisema Juma aidha juma amewaombawakazi wenzake kulitumia daraja hilo kama kivuko ili kuepusha ajali “Nawaombawakaziwenzangutulitumie daraja kuvukia ili tuepukanae na ajali” alisistiza juma
Naye mmoja wa madereva wanaotumia wanaotumia barabara hiyo Musa Hussein ameliambia chipukiza kuwa wao kama madereva imewasaidia kuendesha gari kwa usala na utulivu kutokana na uwepo wa daraja hilo linalotumiwa na watu na kusababisha kupungua kwa foleni “kwa upande wetu imetusaidia kuendesha gari bila hofu na pia foleni imepungu tunashkuru” alisema Hussein

Hatua ya serikali ya kueka daraja katika eneo hilo imepongezwa sit u na wakazi bali wadau kutoka sekta mbalimbali kwani kumepunguza ajali za mara kwa mara zilizokua zikitokea katika eneo hilo.







No comments:

Post a Comment