Thursday 27 October 2016

Vijana wataka kuwezeshwa katika michezo.


NA Daud alex
Vijana wa mtaa wa kilungule kata ya kilungule jimbo jipya la mbagala wameiomba serikari ya mtaa wao kuwaunga mkono katika mchezo wa mpira wa miguu ili waweze kukuza vipaji vyao katika mchezo huo kwani unapendwa na vijana wengi.
 
Akizungumza mmoja wa vijana wa mtaa huo Majidi nduli ameiambia safari255 kuwa katika mtaa wa kilungule kuna viwanja vitatu ambavyo vyote hujaa wakati wa jioni kwa kufanyiwa mazoezi ya mpira wa miguu hivyo hiyo ni ishara kuwa mchezo huo unapendwa sana.
 
Aidha kwa upande wao wakazi wa mtaa huo wamesema kuwa vijana wengi wanapenda mchezo huo hivyo wanaiomba serikali ya mtaa wao kufanya jitihada za kuhakikisha wanawaunga mkono vijana  ili kuweza kuwaepusha na vishawishi  ambavyo vitawatia hatarini.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa huo Barnabas Kayuni amesema kuwa serikali yake imejipanga ipasavyo ili kuyaomba mashirika binafsi pamoja na wananchi wa mtaa huo kuanzisha ligi mbalimbali ili waweze kufanya uhamasishaji kwa vijana hao kwani serikali ya mtaa huo peke yake haitaweza.
 

No comments:

Post a Comment