Thursday 27 October 2016

MAZINGIRA WANANCHI WALALAMIKIA MACHAFU

Na Hamisa mkongo
Wakazi wavingunguti katika wilaya ya ilala jijini Dar es salaam wamelalamikia mazingira machafu husussan katika maeneo ya spenko wakidai kuwa hali hiyo inahatarisha maisha na kusababisha maambukizi ya magonjwa kutokana na mtiririko wa maji machafu kotoka katika viwanda hivyo.



Akionesha hisia zake mmoja wa wakazi wa eneo hilo Asia Rashid wakati wa mahojiano maalum na gazeti la chipukizi mkaazi huyo alieleza kuwa wana hofu ya kupatwa na magonjwa kutokana na hali ya uchafu kukithiri “tunahofia kupata magonjwa kwa sababu ya maji machafu yanayotiririka katika viwanda hivi apa vingunguti” alisema Asia.

Kwa upande wake mmoja wa wafanyakazi wa viwanda hivyo Issa Ali aliliambia chipikizi kuwa mindombinu mibovu katika viwanda hivyo ndio miongoni mwa sababu zinazopelekea uchafuzi wa mazingira “viwanda vyetu vimekuwa na miundombinu mibaya ndio maana kunakosekana sehemu yakupeleka maji taka” alisema Ali.

Licha ya juhudi za chipukizi kuwasaka wakuu na wasimamizi wa viwanda hivyo lakini juhudi zao hazijafua dafu.

Kero za maji taka kutoka kwenye viwanda nchini nchini limekua tatizo sugu huku kidole cha lawama kikielekezwa kwa serikali kwakulifumbia macho swala hilo.

No comments:

Post a Comment