Thursday 27 October 2016

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WANANCHI

Na Samiri Mwegero

  Ni muda mrefu tangu wakazi wa maeneo ya Ilala ĵijini Dar es salaam ŵamekuwa wakilalamika juu ya swala la kukosa alama za kivuko cha watembea kwa miguu maarufu (zebra) katika barabara ya uhuru maeneo ya chuo cha uandishi wa habari (Tsj) hasa katika kituo cha msaada garage.




Hivyo serikali imesikia kilio cha wakazi hao na kuweza kufanikisha kuweka alama ya kivuko (Zebra) ili kuepusha malalamiko pamoja na ajali za mara kwa mara zinazotokea katika eneo hilo.



Sameer Kassimu mwegero ni mmoja ya wakazi waishio katika maeneo hayo alisikika akizumzungumza maneno haya alipohojiwa na mwandishi wetu “ Tunashukuru sana kwa serikali kusikia kilio chetu na kuweza kufanikisha suala kuweka alama za kivuko japokuwa kuna uhitaji wa kuweka tuta japo moja ili kuimarisha usalama katika eneo hilo”. 
              

No comments:

Post a Comment