Thursday 27 October 2016

Njaa yaikumba shule ya msingi Laibon

Na Maria Kilua

Shule ya msingi Laibon iliyopo wilaya ya Munduri mkoani Arusha inakabiliwa na tatizo la maji hali iliyopelekea wanafunzi hao kutopata huduma ya chakula kwa zaidi siku tatu hali inayopelekea ufauru kuwa mdogo.

Wakati serikali ya awamu ya tano ikionekana kutoa nguvu zake nyingi katika swala la elimu kwa kuja na mchakato wa elimu bure ili kuhakikisha kila mtoto wa mtanzania analata elimu.


Hali hii imeonekana kushindwa kuzaa matunda kwa shule hii kwani pamoja na kupata elimu bure shule hiyo imekuwa ikikoowa miundombinu ya maji na hatimaye watoto kufikisha hadi nusu hadi wiki bila kupata chakula.

Akizungumza na waandishi wa habari kutoka Chipukizi mwalimu mkuu wa shule hiyo ROGATH MBUYA ameiomba serikali kuitazama kwa jicho la pili kwani tatizo hilo halipo kwa wanafunzi tu bali hata walimu pia.
                                      

Licha ya changamoto wanzokutana nazo watoto hao bado wana ndoto na lengo makubwa kama vile udaktari, urahisi na mawaziri lakini ndoto hizo zimekuwa zikififia kila uchwao kutokana na changamoto wanazokumbana nazo katika masomo yao.



Wanafunzi hao kupitia uongozi wa wanafunzi wameiomba serikali ya wanafunzi wameiomba serikali kutazama changamoto zinazowakabili wanafunzi katika shule zao hususani zile za vijijini kwani zinaonekana kusahaulika.

No comments:

Post a Comment