Wednesday 26 October 2016

WANANCHI WAFURAHI NA UKARABATI WA MTO BUGURUNI MALAPA


NA HIDAYA YUSUPH
Dar es salaam
Wakazi wa maeneo ya buguruni malapa jijini Dar es salaam wamefurahia ukarabati  wa mto unaoendelea katika eneo la buguruni malapa ambao umekuwa ukisababisha mafuriko na mmomonyoko wakati wa mvua nakuleta adha kubwa kwa wananchi wa maeneo ya jirani.
Mwonekano wa mto wa buguruni malapa kwa sasa wakati ujenzi ukiendelea


Wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema mto huo kwa mda mrefu umekuwepo bila kufanyiwa ukarabati na imekuwa ni hatari kwao kwakuwa mara nyingi mto huo umekuwa ukijaza maji na mara nyingi kusababisha mafuriko katika maeneo hayo

Wamesema wakati wa mvua kuwekuwa na kero za mto huo na umekuwa ukimonyonyoka kwaa kasi zaidi pembezoni  hali iliyokuwa ikitishia kubomoka kwa nyumba zilizojengwa katika maeneo jirani  na mto huo kwa miaka ya baadae.
Ukuta mpya unaojengwa kwajili yakuzuia mmonyonyoko kaatika maeneo ya jirani na makazi ya watu walioko jirani na mto huo


Kwa upande wake mwekiti wa eneo hilo amesema ni hatua kubwa kwa serikali kuanza kutimiza ahadi walizotoa kwa wananchi nakuongeza kuwa tatizo ilikuwa ni ukarabati wa mto huo kutowekwa kwenye bajeti zilizopita.

Amesema ukarabati ni kwaajili yakuepusha adha ambazo zingesababishwa na mto huo kwa miaka ya baadae hasa wakati wa mvua ikiwemo magonjwa na mafuriko ambayo ni hatari kwa maisha ya wananchi.
magari yakiendelea na matengenezo katika mto wa buguruni malapa


Wakati safartz255 inajaribu kumtafuta mkandarasi wa daraja jitahada ziligonga mwamba kwakuwa mkandarasi hakuwa tayali kuzungumza kuhusu ujenzi huo kwa sasa.
Alama za tahadhari katika eneo la ujenzi zinazowekwa na watu wa usalama na afya makazini


No comments:

Post a Comment