Wednesday 26 October 2016

VITENDO VYA UHALIFU VYAZIDI KUONGEZEKA DAR.

Na Victoria Patrick

Kamanda wa polisi kanda ya maalumu ya jiji la  Dar es salaam kamanda Simoni Siro akiongelea hali ya usalama jijini.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, jana amethibitisha hali ya usalama ni nzuri na jeshi hilo limethibiti vitendo vyote vya uhalifu vilivyoibuka hivi karibuni.

Pia alizungumzia suala zima la vijana wanaojiita panya road, wanaosumbua jamii kuwa linashughulikiwa kikamilifu.

“hawa panya road lazima tuwatie nguvuni hawawezi kusumbua jamii”alisema kamanda siro
pia amevitaja baadhi ya vitendo vya uhalifu vilivyokuwa vikitawala jijini humu kuwa ni pamoja na wizi, ubakaji na utapeli.


Aidha kamanda siro amesema jeshi hilo limeimarisha ulinzi katika maeneo ya yote ya jijivhususani nyakati za usiku ili kukabiliana na matukio ya uvunjifu wa amani.


No comments:

Post a Comment