Temeke Market ni timu chipukizi
ambayo imepata jina kutokakana na mechi za Ndondo CUP ambayo ligi zake zilimalizika
mwezi Agust 2016 na kupata ushindi wa kombe katika kuingia fainali na kuwa
mshindi wa kwanza katika mechi hizo.
Vile vile temeke market ilicheza
mechi ya kirafiki na Kauzu Fc katika uwanja wa karume jijini Dar es salaam na
kuwapa mshangao mashabiki wao kwa kuwalaza mbele kwa bao 3-1 ushindi katika mechi ya kirafiki.
Hata hivyo kwa upande wa
mashabiki wa kauzu Fc walizungumza kuhusiana na kipigo hicho ni kutokana na
mazingira na kutokujipanga kwa wachezaji lakini wanaimani na timu yao kwa
asilimia kubwa kuwa mchezo mwingine watafanuya vizuri.
Mchezaji wa timu ya kauzu fc
alizungumza na mwandishi wetu kwa kusema ni kweli wamefungwa na wamepata kujua
nini wanatakiwa kuongeza katika kufanya mazoezi lakini pia ni jambo ambalo
halitojirudia tena.
Kocha wa timu ya kauzu fc alisema
wanahitaji ushirikiano Zaidi katika kuendelez vijana ili kufika mbali katika
kulisakata soka la Tanzania na kupata fursa ya kucheza na timu kubwa ili kupata
uzoefu katika viwanja vya nyasi na hiyo yote ilikuwa ni mara yao ya kwanza
Kocha wa timu ya Temeke Market Mgaya Ally alimalizia
kwa kusema anawapa mazoezi makali wanafunzi wake na anamatumaini ya kufika nao
mbali ila wanauhaba wa viwanja na kuiomba serikali kuweza kuwaboreshea viwanja
na kupata uzoefu ili kuweza kucheza na timu kubwa kama Yanga, Simba na
nyinginezo.
No comments:
Post a Comment