Thursday 27 October 2016

MITARO YA MAJI TAKA YAWALIZA WAKAZI BUGURUNI KISIWANI



Na Janeth frank
          
          Baadhi ya wakazi  waishio buguruni katika manispaa ya ilala jijini dare es salaam walia na miundo mbinu ya kupitisha maji taka kati mtaa wa buguruni kisiwani ambapo makazi ya watu yapo karibu na mtaro huo. 


huu ni mtaro ambao umepita katika mtaa huo unaoelekea sukita picha na janeth frank
                                               



        Wakazi hao wamesema kuwa katika mtaa huo wa buguruni kisiwani kuna mtaro mkubwa unaoelekea maeneo ya sukita , kitu ambacho kinasababisha uchafuzi wa hali ya hewa kuwa mbaya hasa nyakati za usiku kwa waishio maeneo ya karibu 
.
         Chanzo cha habari cha safaritz kilizungumza na baadhi ya wananchi hao ,ambapo mmoja wao aliyejitambulisha kwa jina la Harid juma alieleza kuwa mara nyingi baadhi ya wakazi helekeza mitaro ya  choo kati mtaro ambao unaelekeza maji hayo maeneo ya sukita 




 
moja ya bomba la choo lililoelekezwa kwenye mtaro huo  picha na janeth frank

.
        Kwa upande wake Bi fatma Adam ambaye ni mfanyabiashara wa vitafunwa kama maandazi ,alisema endapo mtaro huo hautafunikwa utaleta madhara kwa watoto ambao hupenda kucheza karibu na mtaro huo mda ambao wazazi wao wanapiokuwa kazini
.
         Aidha bwn geofrey lyanga naye kwa upande wake  alieleza jinsi ambavyo anakerwa na harufu mbaya ya mtaro huo na kuiomba serikali kufanya utaratibu wa kufunika mtaro huo ,kwani unaweza kuwa ni chanzo cha magonjwa ya mlipuko.


 
Moja kati ya makazi ya watu ambayo yapo hatarini.
         



          Chanzo cha habari cha  safaritz kilifanya jitihada za kuutafuta uongozi wa hususani mwenyekiti lakini ziligonjwa mwamba, lakini mjumbe wa mtaa huo alikiri kuwa amepokea malalamiko hayo kutoka kwa wananchi hao na alifikisha kwenye uongozi wa juu.

No comments:

Post a Comment