Friday 28 October 2016

WABEBAJI TAKA WATELEKEZA TAKATAKA VINGUNGUTI



NA MSAFIRI  MOHAMEDY

    Kampuni Asman Ltd iliyokuwa imeshika tenda za ubebaji  takataka katika eneo la vingunguti kombo wametelekeza takataka zilizokusanywa katika eneo moja ambalo hutumiwa kwa kukusanyia taka hizo na wao huja kuzibeba kwa sababu ya wananchi kugoma kutoa hela za kugharamia huduma hiyo.

 



    Yamezungumzwa hayo leo na mmoja wa  wafanyakazi wa kampuni hiyo na kusema kuwa imewabidi wasitishe kutoa huduma hiyo kwa sababu kuwa idadi kubwa ya wananchi wengi hawakotoa kiasi cha shilingi 1500 ambayo hutozwa kwa ajili ya huduma hiyo kwa kipindi cha mwezi.

    Mwenyekiti wa mtaa huo  amesama kuwa wapo katika mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo   ili waendelee na kukusanya taka katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuongea na wananchi ili wawe wanatoa pesa ya kulipia gharama hyo kwa wakati sahihi ili kuondoa mvutano baina ya wananchi na kampuni hiyo. 

   Pia wanachi wanaoishi na maeneo karibu na maeneo ambayo takataka zimetelekezwa waliuomba uongozi wa eneo hilo kulishughulikia tatizo hilo haraka iwezekanavyo ili kukinga afya zao kwa sababu ya harufu kali inayotoka kwenye takataka hizo.

    Mwenyekiti wa eneo hilo aliongezea jambo kwa kuwataka kuwa wasikivu na waelevu wanakuwa wanatakiwa kuchangia au kujitolea kitu katika jambo lenye manufaa kwao na jamii kwa ujumla.
   Mpaka mwandishi wa habari hii inaondoka eneo la tukio hapakuwa na makubaliano ya   viongozi wa mtaa na wale kampuni iliyoshika kazi ya kuzoa takataka katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment